Tierfabeln und andere Erzählungen in Suaheli: Wiedergegeben von Leuten aus dem Innern Deutsch-Ostafrikas [Reprint 2019 ed.] 9783111638898, 9783111256306


187 72 6MB

German Pages 120 [128] Year 1910

Report DMCA / Copyright

DOWNLOAD PDF FILE

Table of contents :
Vorwort
Texte
Übersetzungen
Recommend Papers

Tierfabeln und andere Erzählungen in Suaheli: Wiedergegeben von Leuten aus dem Innern Deutsch-Ostafrikas [Reprint 2019 ed.]
 9783111638898, 9783111256306

  • 0 0 0
  • Like this paper and download? You can publish your own PDF file online for free in a few minutes! Sign Up
File loading please wait...
Citation preview

Archiv für das

Studium deutscher Kolonialsprachen. Herausgegeben von dem

Direktor des Seminars für Orientalische Sprachen

Prof. Dr. Eduard Sachau, Geh. Oberregierungsrat.

Band XII.

Druck und Kommissionsverlag von Georg Reimer. Berlin 1910.

Archiv für das Studium deutscher Kolonialsprachen.

Band XII.

Tierfabeln und andere Erzählungen in Suaheli wiedergegeben von

Leuten aus dem Innern Deutsch-Ostafrikas,

gesammelt von

Gebhard Lademann, O b c r l t . i. Inf.-Regt. Nr. 26

übersetzt von Assessor L u d w i g K a u s c h und Assessor Dr. A l f r e d Reuß.

D r u c k und K o m m i s s i o n s v e r l a g v o n G e o r g Berlin

1910.

Reimer.

Vorwort. D i e meisten der folgenden Tierfabeln und Erzählungen h a b e ich mir von Eingeborenen diktieren lassen. Ein kleinerer Teil

ist

von

einem

früheren

Schüler

der

Mission Kisserawe niedergeschrieben worden. keinen

Anspruch

auf

ein

grammatisch

evangelischen Sie

machen

richtiges

Suaheli.

F a s t alle Erzähler stammen aus Ukami und K u t h u , sind nur vorübergehend

an

der K ü s t e

gewesen

Suaheli nicht als Muttersprache.

und

sprechen

D i e Erzählungen

das

bringen

also ein Suaheli, w i e es der im Innern reisende oder tätige Europäer meist hört. Ich bin Herrn Prof. Dr. V e l t e n zu großem D a n k e verpflichtet, daß er die Übersetzung und den D r u c k der Erzählungen veranlaßt und die große Mühe nicht gescheut hat, die Aufzeichnungen

zu

sichten

und

die

Rechtschreibung

auszugleichen. Die Übersetzer treffen den naiven T o n der Erzähler in glücklicher Weise.

Ich spreche beiden Herren meinen herz-

lichsten Dank aus, daß sie die mühsame Arbeit, zu der mir die Muße fehlte, übernommen haben. N e u - B a b e l s b e r g , Februar

1910.

G. Lademann.

Texte.

Texte. 1. Habari za Bushiri. Bushiri anapita anakwenda Kilossa, halafu Mpapwa. kutoka Mpapwa anakwenda Iringa anapiga shauri na Wahehe na Wahehe wamekataa. anaondoka Iringa anakwenda Luipa, nyumba ya Wambunga. anapiga shauri ya vita, anamwambia yule Ndwangira: » Wazungu wanatazama macho juu, tutawapiga marra moja tu.« halafu vita inakusanya inataka kwenda pwani. iena tunaondoka, halafu tunapiga kwanza Mgeta, halafu tunakwenda Ruvu kwa Kirundira, tena tunakwenda Fisiga tumepigana na Msaramo Sumarokwale. tunatoka tunakwenda Yombo. siku ya kwanza doria waliwaua Wanyamwezi tu, walikata kuni kuuza mjini Bagamoyo. na siku ya pili tunaondoka, vita yote inakwenda inapanga Yombo ndani ya mashamba ya mhogo. pamoja na miti miembe na minazi ya Yombo iko karibu. na ndani ya vita kabila nyingi. kabila moja Mudamba inatoka mtoni Ulanga, kazi yao kuvua samaki, wanachukua mikuke, miti yake milanzi. wengine wanachukua bunduki. Wapogoro walichukua mishale, Wakutu bunduki. Wambunga wenyi ngao kubwa, ngozi yake nyali na mikuke midogo mitatu na mkubwa wa nne na muhimbati 1) wa mkole 2). mkubwa wa vita tunaita likosse na fina lake Ndwangira, na likosse Ungine Nyalioto. Ndwangira mnene mlefu, Nyalioto mfupi mwembamba. walipiga zamani vita ya Wandamba. Wandamba waliangukia, wengine wameuzwa pwani, na tena wamepiga na Wakutu wa humu Kisaki. na Kamwamka likosse la Wagogo wa > in chi Songea. zamani alimwua Mwarabu jina lake Songoro Bange, alichukua mali mengi na meno ya tembo. sasa wandu woha wahangalana kuwingai) Wazungu. Bushiri anasema: Wazungu wabaya, watumwa watawandikia, wataharibu inchi, tuwapige waondoke, mtapata mali mengi ya nguo. na wale •) Keule. *) . . . baum. 3) = wallt u'ole walichanganya A r c h i v f. d . S t u d . d e u t s c h . K o l o n i a l s p r .

kujukuza. Bd. XII.

1

2

Wambunga walisema: warungwana wanatoka ngambo. na Bushiri anasema: wale wakorofi sana, ifaa kuwapiga wakimbie; na antri ilitoka kwa sultani Saìdi, ananipa bunduki na baruti, anasema: kama mwenyi nguvu upigane nao. Nussu ya watu walikwenda polini kuwafuatia watu, kwenda kuwakamata, wanamme kuwaua na wanawake kuwakamata pamoja na watoto na mali kuchukua. Bushiri alikataza alisema: kwanza tupigane na Wazungu. na wale Wambunga wanakataa wanasema: sisi tutapiga tu. wote tutaua, walituletea nini? kazi yetu kuua watu tu. Na halafu saa nane Mzungu anakuja pamoja na kompania ya wanjolinjoli1). tena tulipigana na yule Mzungu, walikufa watu mia u khamsin. bunduki moja kwanza na halafu tatù marra moja. sisi hatukujua, tulizannia milanzi inapasuka. Bushiri alisikia bunduki zinalia, alipanda marra moja juu ya punda maskati mweupe. halafu anakimbia, hakusimama, hakupiga hatta bunduki moja. na wale wafuati wake hawakupiga walikimbia tu. halafu askari wote wa Mzungu wanjolinjoli walipiga feuer marra mbili, na halafu schnellfeuer. walipata, na sisi tunazidi kwenda. tunakimbia tunakwenda Ruvu. na kule Ruvu yuko Mzungu juu ya nyumba, anapiga bunduki katika saa senashara ya usiku. na watu wengine walikufa na maji mtoni Ruvu. tena tunakwenda Mangomole juu ya Ruvu. tunàfanya shauri kumwua Bushiri. na yeye amekwisha kukimbia njia ya pekeyake, amekwenda Uzigua pamoja na watu wake. Na sisi tunarudi. killa watu wanakwenda kwao tunajikaa. twalikimbia kwa ile bunduki inatatalika kama mhindi wa kukalanga. kama ile bunduki ya zamani ya kushindilia kwa mdomo tungeweza, tungewaua wote. wanjolinjoli wandu kidogo ngalituwakomite woha, sisi twenga twa mahere2). — tumekaa mwaka moja amekuja Msaramo Kawamba Mshale kupiga vita yake. twalimkimbiza. Tena mwaka ule akaja Mzungu pamoja na kompania hapa Kisaki, jina lake bwana Schmidt. wakubwa walisema: tupigane. watoto walikataa, walisema: hawa wabaya, ile bunduki hapana kuweza kupigana. mwache apige aondoke, na sisi tutarudi. tutakimbilia juu ya vilima, hapana kufuata. alishinda siku moja, alipiga mayumba moto, alipata kuku tu na njiwa bassi, mbuzi hakupata na watu hakupata. asubuhi aliondoka. ') Sudanesen; njolinjoli *) = wengi sana.

=

Beinbinden.

3 Tena tunajenga tunakaa tunalima. mwaka ule sawasawa kama walipiga bwana Schmidt akaja bwana Nyundo l), alitoka Kilwa pamoja na kompania kubwa sana na mzinga moja ulichukuliwa na wapagazi. alifikia kwa Hongo -), alileta habari alisema: sasa wale Wambunga ninawataka tupatane, na miye sitaki kupiga. ninatafuta wakali zayidi. halafu tukapatana, alikuja kujenga ngambo ya Mgeta 3), sababu watu wengi watanyanganya chakula. na asubuhi shauri ya kumwonyesha Iringa. hapa alichukua kirongozi Tarange, alikwenda naye mpaka Mgoda, inchi Kilossa, Tarange alirudi. Na bwana Nyundo Wahehe walimzuia njiani, mtwa wao sultani Kwawa aliwafisika watu wake ndani ya mayani, marra waliruka, wakachanganyika tena, sababu karibu, walipiga bunduki nyingi sana. na Wahehe walikufa zayidi ya askari. wote walichoka, Wazungu wanachoka, na wale Wahehe wamechoka. Mbunga Abdallah aus Kimki.

2. Habari

za

Wambunga.

Zamani kazi ya Wambunga kupiga vita tu, na wale kukamata ndio mali yao. Wakutu waliwaita Wambunga Mafiti. Vita ya zamani kama mangia hapa Kisaki, tuhambe*), na tena inakwenda itakaa kama kwa Mgunda 5), na halafu tutakwenda usiku tutafika kama Kirengwe b). tutatuma watu watano, watakwenda kuangalia mji. halafu wale wataleta habari watasema: watu wamelala wote tena jogoo ya kwanza tunajongea karibu sana, na saa kumi na mbili asubuhi vita inaingia. wanamme hapana kuwakamata, kufa wote, sababu nguvu. wanawake kukamata na mibuzi kuchukua, na halafu kama wale watu wakaidi kupigana, tena wengine watasema: tukimbie. na wengine watalala chini ya majani. watu wa mjini wanafuata, na ivale watu wa vita nussu wanakimbia, na wengine wanalala chini, wanakuja karibu, wanapiga mikuke, na tena wale wanakufa zayidi wanakimbia. ') *) 3) *) S) b )

v. Zelewski. Jumbe in dt r Nàhe voti Kisaki. Name des Flusses, an dem Kisaki — lunaondoka. Ori. 12 Std. v. Kisaki. Ori, 4 Std. v. Kisaki.

liegl.

Kwetu inchi yetu kubwa ngombe mingi na ulesi ') mingi chakula yetu, na kalanga nyingi na pombe ya mianzi na ndizi juu ya mtoni Lutukira. unatoka kilima cha mbunga, unateremka tena unakutana na Nyassa bahari kubwa. Lutukira haukauki mwaka mzima hatta miaka yote. na vita yalipigwa na Mputa mwenyi watu wengi, walikuja na ngao ya ngombe ya mjini, na juu walivaa manywele ya kajolagongo -). tena walipiga miji yetu na ngombe walitunyanganya yote. halafu tuliangukia twaliwafuata amri yao. tena wakubwa alikuwa anawachincha, anataka kubakiza watoto watupu. na wakubwa wengine walikuwako walikasirika walisema: »tumpige, huyu mbaya.« yule Afputa alikwenda Manguru na tena Manguru alikufa juu ya vita, tena watu wake waliongoza njia ya kwao. Na sisi twalibakia juu ya miji. halafu alikuja mwingine tena Kipeta hatta sasa iko Songea. walipigana naye; lakini kabila yetu yalikimbia, alitufuata, yeye nyuma na sisi mbele. sisi tuwalipiga inchi ya Wandwere. Wandwere walikimbia twaliteremka tunafika tunapiga inchi ya Mujera. na yule Kipeta alitufuata alifika Mujera alipiga alikamata watu wengi zayidi na wengine wengi walikufa. alirudi nyumbani kwake alipata habari ya vita na Mjugum.be alikuja alipiga inchi yake alikufa Kipeta. ya pili mtoto wake Kipeta alifanya vita kubwa anakwenda kwa Mjugumbe alifika walikutana njiani walikufa watu wengi kabisa. na yule Mjugumbe walimpiga mkuke na mkuke mwenyi meno yake manne na ile ncha ya mkuke ya tano. alipata mkuke wa mbavu. alikimbilia juu ya jiwe yenyi shimo kubwa. na halafu vita yalipiga mji wake wote yalinyanganya ngombe nyingi na mbuzi nyingi, kuku hapana. na wao chakula umbwa wa mjini. munga AbdaUah atts Kisaki.

3. Habari za Wakamba. Wakamba walifanya urafiki na Njalioto i), kazi yao kulasa tembo pamoja na kiboko na kifaro na nyati, punda, kongoni, nsewei), bunzuS), tandara 6J, parapi '). halafu waliua tembo ') Kleine Hirseart, Eleusine. *) Dunkler Wasservogel (schwarzer i) Häuptling der Wambunga. *) Gelber Riedbock. 5) Elenantilope. ) Kudu. 1) Pferdeaniilope, sowohl helle als

Ruhir?).

dunkle.

5

nyingi, alipiga shauri alisema: nitawaua niwanyanganye mali yao. na yule mkubwa wa Wakamba Ngarawa aliuawa. na Njalioto alimnyanganya tembo, na Wakamba walikufa wakumi na Wakamba wanane walikimbia, walipeleka habari kwa sultani yao Mkamba inchi yao Mangubugubu. na sultani yao alisema: ndio male Wambunga mkiwaona — vita, sababu wametuua, ita sisi walikuwa warafiki yetu na sasa wabaya. tukiícaona kufa tu; lakini kwanza kituliza: wee nani? naye kisenia: Mbunga, mpige mshale, kama kabila ingine bassi, hapana kupiga. na Mkamba ikenda, killa mtu njia yake kukutana kambini. kama analasa killa mtu atakuja kutoka penyi nyama. na nyama yao kuchukua kichwani, na asubuhi killa mtu njia yake kukutana kama kwa Mgunda1). atatangulia mtu moja penyi kambi, na wote watafuata ile kambi, hapana kupotea. na wakilasa nyama, kulla siku moja, ya pili hapana kuchukua. yote itatupwa palepale. na mtu ukitaka kuomba, uombe: dilumba wana Wakamba. ukiomba mino ja hupati. yule mmojá atakupa kadiri yako, maana yake: umezarau Wakamba, sababu hukujua sisi Wakamba tunalasa wote. Wakamba wakafika penyi tembo, killa mtu atasimama, ivanapima mishale yao kwa juu. na ikitoka ile mishale wanasema: nimelasa mwana Mkamba. na malembo wanakimbia, na killa mtu anatangulia. lakini killa mtu anajua alama ya mshale, teña wanakamata nyama ya mkonga. kula kwao nyama tu, hapana kutokea penyi mji, hapana kazi yao, wakipata nyama — bass. na kama usiku iko pekeyake atakwenda kama simba, sababu anaogopa poli, tena anawakutana wenziwe penyi kambi. na humu polini hawezi kukutana na watu wa Wazungu. na ukikutana umwambie maneno mazuri, úseme: mimi mtu wa bwana mkubwa. na ikikuuliza: unataka nini polini? mwambie: nataka nyama tu. na ukisema: nataka tembo tapiga mshale na yeye atakwenda. Na tena kama anakwenda safari anachukua dilonge2) pamoja na upinde na migulu ana funga kamba ya ngozi inatengenezwa kwa uzuri, anafunga juu ya miguu mpaka wa níafundo. Mbunga AbdaUah.

•) Ort, 12 Std. v. Kisaki. V Kócher.

6

4. Hadisi ya rribu no, baridi. Zatnani ezi ya Seliman bin Daud walishuka mbu walikuwa kama ngamia, wanauwa watu na nyama ya polirli, halafu nyàma wakenda kwa baridi kushitaki kama: mbu wanatuua burre. baridi ikenda kwa sultani kutaka amri kuwatafuta mbu hao, wanaua nyama burre. ikataka rukhsa, ikenda katika pori kutafuta mbu. baridi inavuma kama tufani, 1) mbu hawawezi kusimama, wanakufa wengi, wakenda kushitaki kwa sultani: baridi inatuua burre. wakaambiwa: kaeni tukaite baridi. ilipokuja baridi kwa sultani, mbu wakàkimbia. baridi akamambia sultani: mimi nimekuja. sultani akiweta mbu, na mbu wakasema: kusimama nguvu zako. sultani akasema: siwezi kuhukumu, maana kulla mtu aliomwua mbu pamoja na nyama ya polini. nimemtuma baridi kumwita mbu, mbu hawezi kuja na sultani akasema: hukumweza haikuwa hatta leo. ambapo mbu na baridi hokumuhii, ndio habari. Stilim bin Jumaa Toki Magogoni (Kisaìci).

5. Hadisi ya Seliman bin Daud. Wakati wa sultani wake muungu alimpa ujuwi wa kujua maneno ya ndege na nyama ote walio katika barra na bahari na majini, na maneno ya baridi yote na maneno ya miti na maneno ya mashetani na samaki wa barra na bahari. halafu akafanza kwa watu wake yule nabii Seliman bin Daud. Akaamru kujenga mayumba ya askari wake kulla nyama wa barra kuja kufanya kazi kuchukua mawe na udongo. Tembo akamambia: mimi mtu mkubwa, sitafanya kazi, nitawatuma watu wangu kuja kujanya kazi kwako. wakaja watu wa tembo kuchukua mawe na udongo, na majini wakatengeneza viwanja, iliojenge mayumba ya askari. waketwa na ndege kuja kujenga nyumba zoo ndege na mkubwa wao elhudhud. halafu elhudhud akaleta ndege wote kuja kujanya mayumba yao wenyewe. na kulla siku ya baraza ya hokumu wanakuja ndege wote kusikiliza hokumu, na majini vi levile, na kulla nyama wanakuja kusikiliza hokumu. siku ya baraza tembo wakaja kumshitaki nabii Seliman, wakamshitaki kwa nabii Daud. wakamwambia: mtoto ')

Sturm. hokumu

yao

haikwisha.

7 wako ametupa kazi nyama wote; sasa tunalumika pekeyelu, na nyama wote hawatumiki. aketwa ngamia akaambiwa: wee kesho utampokea tembo kazi. ngamia akasema: mimi kazi yangu ninatoa maziwa, wanakunywa wafanyaje kazi. aketwa ngombe akasema: mimi ninatoa maziwa anakunywa nabii Seliman. halafu aketwa putida wakaambiwa: kazi yenu kuchukua udongo na mawe. panda akakirri. tembo akapata rukhsa. panda wakajanva kazi siku nyingi. halafu punda wamechoka, wakamwambia ngombe: sisi tumechoka sana kwa kazi, na sisi tunaogopa kumwambia kweli sultani, na sasa tunataka akili kwako. ngombe akamjibu punda, akamambia: mimi nitakupa akili; lakini usimivambie mia mwinginewe, ukamwambia utanichongea mimi kwa sultani, kesho asubuhi wakaja wachunga nie ole punda jitieni ugonjwa. na sultani anasikia maneno yao va ngombe, anamfundisha akili punda. asubuhi walipokwenda wachunga, punda ivamelala wote, wamejitia ugonjwa. wachunga wakarudi kwa sultani, wakampa habari punda wote wagonjwa. sultani akaamru kuchukuliwa ngombe ivate kuchukua mawe na udongo. halafu mtoto wa sultani na waziri iva sultani wakamwambia sultani: kwa nini ngombe wanachukua mawe na udongo? sultani akawajibu: kwa nini mkaniuliza? wakamjibu: sisi maziwa tutapata wapi ya kunywa? akasema sultani: mtakunywa maziua ya ngamia. ngombe akatumika mwezi mmoja, akaona taabu nyingi, akamambia punda: weye rafiki yangu nimekupa akili; kesho ondoka unipokee taabu hii niliyo nayo. punda asimjibu neno, akajitia ugonjwa. halafu ile ngombe akatumika siku saba, akamwambia punda: mimi nimesikia maneno kiva sultani, kama kesho hukuondoka utachinshwa. na sultani amekaa na mkewe pamoja, sultani aliposikia maneno ya ngombe, akacheka. halafu mkewe akamwambia: unacheka nini? mume wake akamambia: sicheki kitu. mkewe akamjibu, akamwambia: kweli neno uliocheka. akamambia: nimekumbuka maneno ya ulimwengu. akamwambia: niambie maneno gani uliokumbuka? na sultani akaona haya na moyo wake kusema maneno ya uwongo, na mke wake akamjibu: kama huwezi kuniambia maneno uliocheka bassi na sultani anampenda sana mke wake,' utaniacha sikutaki. akamambia: nataka mudda siku saba nitakupa majibu. mwanamke akamwambia: sikubali, utanacha. na yeye nabii Seliman akamambia: ngoja nisali rakaa esnin, nitakuambia maneno niliocheka. alipokwisha kusali, akaweta nyama wote na samaki wote na watu wote na majini wote, akawaambia: mimi nime-

8 gomba na mke wangù; nataka mfanye maneno tupatane. watu wale wakamwambia mwanamke wa sultani: upatane na mume wako. mwanamke asikubali: kama anataka tupatane, shurti aniambie neno aliocheka. na sultani anaogopa kwa muungu amemwambia maneno niliokupa kujua maneno ya ndege na nyama wote na majini ote ukamwambia mtu, utakufa. watu wakashindwa kuwapatanisha. halafu sultani akaweta ndege wote, na ndege wakashindwa vilevile. halafu akaweta majini yote, wakashindwa vilevile. halafu sultani akapotewa na akili, na watu wote na nyama ote na kulla kitu katika dunia wameangiwa na msiba, ya kuwa atakufa sultani wao. halafu ilipokuwa alfajiri, majogoo wakawika. umbwa wa sultani akaingia kuwakamata majogoo. sultani alipoona, umbwa anakamata majogoo, akamwuliza umbwa: sababu unakamata majogoo? umbwa akamjibu, akamwambia: hawa majogoo hawana haya, kulla kitu katika ulimwengu kina msiba ya kufa weye sultani, na jogoo anawika, hana horuma yako weye sultani, jogoo akasema: sultani hana akili, mimi wanawake wengi mtu mmoja katika wake wangu, akajivuna mmoja humpiga, na yeye sultani mke wake mmoja anamshinda, anataka kufa kwa sababu ya mwanamke. angalikamata bakora, akampiga angalitubu asingalitaka maneno aliocheka. sultani aliposikia, akakamata bakora, akampiga mwanamke, akamwambia: nimetubu, sitaki neno uliocheka. wakafurahi watu wote kwa kupona sultani wao kwa akili ya jogoo. — „ ,. .. T J

1

o

Saltm bln Jumaa.

6. Maskini na tajiri. Maskini na tajiri wa hapo zamani. tajiri ana mji wake na maskini ana mji wake bassi, maskini na ngombe wake tajiri atamani ngombe ya maskini. na maskini akanena: chinja ngombe, nyama kula, ngozi nipe mwenyewe. tajiri akampa ngozi. maskini akanena: hakuna ujinga kana tajiri; akanipa mali Jvaneu. ° Ifkami Salande Mn Kida Ktaanga bei Tununguo.

7. Mtu

mwenyivu1).

Mtu mwenyivu akajenga mna polini pekeyake kwa sababu ya bibi yake yasitongozwe na mwanamme. hatta siku moja ')

Eifersüchtig.

akaja fundí mpiga nyama. akabisha hodi. mwanamke akasema: karibu. bassi tena akanena sababu ya kukaa hapa porini nini? mwanamke akanena: mimi mwanamme wangu ana wivu sana, funài akamzini nayo. bwana alivorudi akamkuta fundi ndani ya nyumba. umbela«1), akanena, wanawake haifai kuwafanyia wivu«. ... . „Hossem ' ' Mkami ìlkobeda

8. Mtu

bei

Tununguo.

mtega mitego na simba.

Mlu mtega mitego ana bibi zake mbili, mwingine mke wa kuposa na mwingine suria. kwenda kutazama mitego akafika simba; amenasa simba, kumwona mtu, simba akanena: meye mtu kwa nini ukatega mtego katika nfia?« simba akamkamata mtu. mke wa kuposa akakimbia, sababu simba ni mkali sana, suria akakaribu kumgombea mwanamme wake. alivorudi nyumbani, suria akanena: »mke wa kuposa hana holuma.« ilkami Kibwana bin MI oro Kisanga bei Tununguo

9. Mbende

saba na udevu.

Mbende saba kazi yake kusaka nyama na udevu kazi yak?, kunyanganya watu. mbende saba akaua nyama wengi sana, udevu akaondoka kwa nguvu na mbende saba akaondoka kwa nguvu wakapigana sana, mbende saba akakimbia sana, sababu ya kuogopa udevu bassi, zamani watu huogopa mbende saba; lakini kwa mwaka mwingine huogopa udevu. bassi ufanye nguvu wachie wenzio. ... ....... „ ö il kann balene bin Bange Kisanga

10.

bei

Tununguo.

Kibwana.

Kibwana na mwalim wake Ali ana bibi. siku nyingi sana akisoma kwa mwalim wake. hatta siku moja bibi yake akanena: »kibwana nini, njoo upesi sana, a kibwana akanena: ma njia nini?« bibi ya Ali akanena: »wewe mjinga sana, hujui kula.v. kibwana akanena: »haya twende.« kupita ndani, akazini na mkewe wa mwalim Ali. kibwana akakosa kazi ya kusoma. Mkami ifguieno bin Sela Kitope bei Tununguo. ')

Schimpjwort

jiir

Wmbcr,

etwa

= Du

Metze

IO

11.

Kibwana.

Mtu mpiga nyama alikwenda polirti akakula nyumba pekeyake, akakuta kijana mwanamke mzuri sana bassi, funài mpiga nyama akauliza: »bibi, wee una mwanamme?« bibi akanena: »sina mwanamme A »sema kwelì. « mwanamke akanena: »lakini baba yangu mkali sana; yakija boba wewe utakwenda na upanga; baba yangu ndiyo atakusifu sana na mimi utanipata.« bassi kibwana asishindwe. Kkumi Lekamba bin Mazengo Kidai bei Tununguo. 12. Ronzi1)

na buwi1)

na

muhangai).

Hapo zamani inchi imekaa usiku na usiku. lakini konzi usiku: »mbona na buwina muhangawakendakwamuungukuuliza usiku kwa usiku sasa? sisi watatu tumekuja kwa kuuliza mchana na usiku.« muungu akanena: »konzi na buwi na muhanga mmepita njia gani?« konzi kanena: »huyo mwenzetu buwi hutungika kamba; muhanga huruka ndani ya kamba iliyotungika buwi; lakini mimi konzi huruka kama ndege.n yeye muungu ataka kukata kamba wapate kufa; lakini muhanga kusikia maneno yote konzi kanena: »muungu sisi watatu tunataka mvua.« muungu akapa pipa kumi za mvua. tena akawaambia, kama mkitaka mchana kachukuwe mijupa ya panya. marra wakashuka chini kufika katikati, muungu akakata kamba. muhanga na buwi wakafa; lakini konzi karuka, akatengeneza mchana. bass. sasa ndiyo maana ùkawa mchana; lakini zamani inchi yote zalikuwa usiku. bassi. iikami (Iniuri ìiin Ali Kidai b. Tumtngtio. 13. Kinegana

tembo.

Kinega na tembo hapo zamani wakagombana na kinega. tembo akanena: »wewe ndege hewani; siwezi kushindana dawa ya ndege mdogo sana A kinega akanena: »udogo si kazi.« tembo ') Fliege. J 3)

2

Spinile. Erd/erkel.

*) Schwalbe.

11

akanena: »haya, íushindane bassi.« »ndege hewani kazi yake kurukaruka.« sababu amepata akili sana.«

14. Sange1) na

ahaja sungura akanena: lembo akasema: Dkweli, Mkami Kipande Kitope bei

bin Kidongu Tununguo.

muhangai).

Sange na muhanga zamani za kale. muhanga na sänge waligombana. muhanga anaogopa kuingia nyumbani mwake. muhanga akaona nguvu za sänge nyingi sana, akanena: »mtu anayomtoa sänge kalika nyumba yangu, atapata rupia 100. kulandi 3 j akanena: »sisi tutamtoa.« marra wakamtoa nje. muhanga na kulandi zamani mtu na rafiki yake. Mkami Knche Kismtgtt hei

hin Jiidogo Titmtnguo.

75. Sungura na fissi. Sungura akanena: Uwende tukatege samaki kica migono«. fissi akakubali sana; sungura mitego yake mbakuna za shingoni na fissi mtego zcake mgono. yule sungura killa siku kwenda asubuhi kwiba samaki za fissi, hatta siku moja fissi akamkuta sungura kwiba samaki za fissi, fissi akamkamala sungura. sungura akanena: »mimi nikamate mkiani unipige ndani ya jiwe nitakufa«. fissi akakubali maneno ya sungura. kumpiga chini ya jiwe sungura akaruka akenda zaka. urafiki ukisha. Chamdn bin Kidole Kidui bei Tunnnguu.

16. Sungura na mwanamke. Sungura akanena: »bibi, ivewe una mwanamme?« bibi akanena: mina mwanamme.« sungura akamwambia: »sisi kwetu tunakula mbuna; lakini kwenu mnakula nini?« mwanamke akanena: »kwetu siye chakula ni nazi na mboga na nazi.« sungura akanena: »mbona maungo yenu si mazuri.« mwanamke akanena: »twende kwenu.« sungura akamtwaa bibi, akanenda hatta kufika karibu na nyumbani. akafika penyi ') Ralle. ') Erdferkel. 1) Ameise.

12 milala, sungura akamkaribisha ndio penyi nyumba?« sungura akalia: »sababu umenipeleka i>kwenu walinikubali, tena huku mirudishe.« sungura akakataa

bibi. bibi akamwuliza: »hapa akanena: màio.« mwanamke polirti?« sungura akanena: unalia.« mwanamke akanena: akasema: »huna adabu. « Mkntu ilagogoni

ìftonga a. Ruvu.

17. Mkopi na Mkulima. Mwàka wa njaa mkopi akenda kwa mkulima. mkopi akanena: mikopeshe kanda 100.« mkulima akampa kanda 100. mtoto wa mkulima akanena: »hawa wakopi si watu wazuri, sababu mkopi akapenda kwa mkulima — verna sana; lakini akanenda kwa mkopi hakupi kitu, sababu mkopi hafi njaa.« zamani mkopi kwenda kwa mkulima kukopa, sasa hapati kitu, sababu mkopi apenda kukopa kwa wenziwe — kwake vibaya. likami Nyambogo

18. Simba

na

bei

Lukengere Tunnngtw.

mbala.

Zamani simba na mbala mtu na rafiki yake. simba akatwaa watoto wa mbala. tena simba akanena kuchukua mzigo huu. njiani simba kusema: mjinga wa mbala kuchukua wanawe mkoba.« mbala akanena: »sasa sitaki urafiki bassi.« mbala akenda kwa umbwa wa mwitu, akamkamala simba, ndiyo maana simba na mbala hawaonani, tena umbwa wa mwitu na simba hawaonani. „, . ,r,, „ Síkamt Matóla Nyambogo bei

btn Tage Tuntinguo.

19. Kibwana na wezi saba. Kibwana zamani kukaa barra, wezi saba kukaa njiani. akachukua kondoo. wezi saba wakanena: »kibwana islamu mzima unachukua panya.« kibwana akanena: »kweli namtupa, afazali kufa na njaa.« kufika kwa bibi yake bibi akamwuliza: )>mbuzi wetu uko wapi?« akanena: »wakaja wezi tuwapige chapa.« aliwapiga chapa wote. kwenda kwa sultani akanena: »watumwa wangu saba hawanifanzi kazi kwangu.« sultani akanena: »kawalete.« kibwana akanena: »sitawaweza.« sultani akatuma askari, wakakamata wezi saba. kibwana akanena:

13

matumwa wangu.« wezi wakasema: »sisi si watumwa, wangwana. kibwana akasema: watumwa wangu wote, wana chapa mgongoni.« sultani chapa akaziona, kibwana akawauza kwa sultani, yeye akapata feza. Mkami Idi Kidni bei

20. Simba na

bin Ali Tununguo.

sungura.

Simba akamkamata sungura. sungura akanena: »wewe simba umenikamata sababu nini?« simba akanena: wewe sungura nimekukamata sababu nikutafune.« sungura akanena: »mimi ukinitajuna hutashiba kabisa«. simba akanyamaza asinene neno. sungura akanena: »simba mbona umenyamaza kimyaP« simba akanena: »mimi nataka nikule. « sungura akanena: »mimi wewe simba nataka nikupeleke pahali kuna nyama.« simba akakubali sana, sungura akampeleka hatta pahali kuna nyama. simba akakamata nyama kumi. alipokwisha kula simba akanena: »sungura ñipe maji ya kunywa. sungura akatwaa maji akatia uchawi akampa. simba akanywa akafa. sababu simba mtu mbaya sana, afazali kufa yeye bassi, sungura mtu ana akili nyingi sana. Situimi Kisanga

21. Maskini na

J I z e h t bin . I / . S Ì I . bei Tununguo.

ndege.

Maskini killa siku kuvua samaki na ndege huwapo chini ya mti. maskini akipata samaki ndege kusema: »maskini nipe samaki.a na maskini akanena: »nikupe wewe samaki mimi nitakula nini?« ndege akanena: mipe tu wewe maskini ukanipa samaki mimi ndege nitakupeleka pahali kuna vyakula; lakini wewe maskini hutapenda kukaa inchi ina vyakula.« maskini akauliza: »kwa nini?« ndege akanena: »sababu maskini hapendi laha.« maskini akabisha sana, ndege akampeleka hatta inchi kuna vyakula. maskini akanena: »sasa mimi nimepata laha bassi.« marra akauliza watu katika inchi ya vyakula, maskini akanena: »mlango wa nyuma wapi?« bibi yake akanena: »mlango wa nyuma mbaya sana.« maskini akabisha sana, tena akamwonyesha mlango. maskini akarudi kwa ndege, akamkuta akasema: »jee, sasa ubishi wako urnekwisha?« maskini asinene neno. Slkami Hutogo Kitope bei

bin Tebe Tununguo.

14

22. Wakami na Waaràbu. Wakami na Waarabu zamani imekaa kabila moja, hatta siku moja wakewe sultani wakapiga akili sana, wakanena: »sultani twapenda tukae barra.« sultani akanena: ornimi nasikia zamani baba yangu kanena: » ukenda barra watu wa pwani watasema Wakami amma Wanyamwezi bassi, tena mtakuwa washenzi, tena mtakuwa watu weusi, hamtakuwa na mali — bassi, hatta nguo za kuvaa mtatafuta hatta chumvi mtatafuta sana.« ndio maana Waarabu na Wakami wakaonana hutaka ufuati sababu zamani udugu wao umoja. Mkami Hntogo bin Tebt Kitope bei Tununguo.

23. Mnyonge1)

na fundi.

Zamani mnyonge hajui kutongoza. hatta siku moja mnyonge akapita kwa fundi, fundi akanena: »weye mnyonge kwa nini hutaki kutongoza wanawake?« mnyonge akanena: •»mimi sijui«. fundi akanena: menda kanunue jaruba.« alipopata jaruba mnyonge akanena: »sasa nataka kwenda tembea bassi, mnyonge marra akaona mkewe fundi yakamtongoza. maana yake mtoto wa mwenzio haifai kumfundiza kazi ya ukahaba, sababu ukamfundiza kazi za ukahaba halafu atazini na bibi yako. sababu fundi na mnyonge. fundi akafundisha mnyonge, alivojua akazini na bibi ya fundi. ifkami

24.

Kinhuhudit bin Sa! eh e Tunungiiv.

Maskini.

Maskini hapo zamani hajui kusafiri, akaja mwewe, akamwambia: mataka uwe rafiki na mimi.« maskini akakubali. mwewe akakuta inchi yenyi miwa. »twende ukakae inchi hii nzuri sana.« maskini akenda inchi ile haina wanàmme maskini akapata laha na wanawake. maskini akafurahi sana. if/carni (hnari bin Dumbu Kikundi kwa .Saffi.

25. Kibwana. Mtu mtoto wake moja, mtoto jina lake Kibwana. baba yake akamwambia: »mimi mwanangu nitakupa rupia 20, ukatafute ')

mnyonge-mjinga.

15 watu wenyi akili.« akakubali. marra baba yake akafa. mtoto akatwaa fesa akenda kwa mtu mwenyi akili akamwambia: mataka akili.«. mzee akanena: mipe rupia 20.« mtoto akampa, mzee akamwambia: meno la sili usimwambie mkeo.« akenda mwituni akaona utango. kurudi nyumbani akasema: »mkc ioangu, mwituni kuna utango.« yule mkewe akanena: mipeleke. ivakenda hatta alipoona utango. wakarudi mkewe akamwambia sultani akenda akakata matango. maana yake hii neno la sili usimwambie mke. Kibwana akanena: »kweli, neno la sili baya —kumwambia mtu, vibava sana.« ,„ . ,. r . -

7

Mfiiimt

htvH'iina

uni

Lnhttnya

THHHWJH".

26.

Mtu

miye

na mvaa

mahuyu.

Mtu miye akanena: »mtu atakayonishinda atapata inchi yangu na watumwa wangu.v. mvaa mabuyu akanena: »mimi nataka nishindane nawe. « mtu miye akakubali sana, icakaweka mashahidi bassi, wakapigana mudda iva siku 10. mtu miye akashindwa ni mvaa mabuyu alyipata inchi ya mtu miye na watumwa wa mtu mive. ,„ . „ , ,. ,,,,,, Mktimt

27.

Svilì hin Titnmigtin.

Abitulhih

Sultani.

Mtu sultani ana watoto watatu, tena amefuga watumwa wengi sana, mwaka moja sultani akanena: »mwaka wa kufa mimi sultani ikija njaa watumwa wote uzeni; lakini nokola msimwuze.« watoto wakakubali sana, baba yao yalipokwisha sema marra akafa. kwa mwaka mwingine ikija njaa wakauza watumwa wote; lakini baba yao alipokufa akanena: watumwa wote mkiuza, lakini nokola msiuze, sababu amekuwa kama marna yenu amma baba yenu. watoto watatu wakakubali sana, tena watoto wawili wanataka kumwuza nokola. yule mtoto mdogo sana akanena: »mbona baba yetu alipokufa ameagiza watumwa wote uzeni; lakini nokola msimwuze. sasa nyinyi mnataka kumwuza. mimi simo sababu na mimi kitoto kidogo nikiuza nokola nitakosa lazi ya baba yetu.« watoto wawili wakanena: »labda wewe unavyo vyakula vingi.« mtoto mdogo asinene neno. wote wawili wakenda kumwuza. kufika njiani wakamwona shetani. shetani akanena: »tema mate.« watoto wawili wakatema mate, shetani watoto akala wote. kitoto kika-

i6 nena: nitawajuata. kwenda njiani akamkuta shetani, kinywa kinawaka moto, púa inatoka nyuki. kitoto kidogo yakamwua shetani, akamtumbua. watoto wawili wakatoka nje. kitoto kidogo kikanena: »sasa mmeona mimi nasema baba yetu akatuambia, watumwa wote uzeni; lakini nokola msimwuze. nyie mkamwuza ndio sababu mkaliwa na shetani, sababu mmekosa lazi ya baba.« BMÍ simba, MAMI Tununguo.

28. Mwongo na mchawi. Mwongo alitaka kushindana na mchawi. mwongo akanena: nhaya nenda.« mchawi akafika mji wa sultani, akaua watu wa sultani hamsini. watu wasiondoke. akarudi nyumbani, mchawi akanena: »mimi mchawi nimeshindwa, sasa nenda wewe. « mwongo akanena: »verna sana.« mwongo akaenda hatta kwa sultani, akamwambia: »wewe sultani ndugu yako Salim analeta vita.«, sultani akanena: »kweli, ndugu yangu Salim mbaya sana.« mwongo akanena sasa karibu ya kupigana sultani na Salim. mwongo akenda hatta ~kwa mchawi. mwongo akamwambia: »mchawi, bado mda wa siku io mji wa sultani utavunjika.« mchawi akanena: »wewe mwongo huna haya. « mwongo akanena: »mimi mwongo kama hakuvunjika nitakupa rupia 10.« mchawi akanena: »na mimi kama ukavunjika nitakupa rupia 10.« mwongo akanena: »kweli, huyu mchawi anataka nile feza yake.« hatta kwa siku ya pili akasikia mji wa sultani umevunjika. mchawi akanena: mwongo si mtu mwema, ukabisha na mwongo utakufa burre bass. ukami Mritho hin Saidi Hoviima kwa

Hembt.

29. Mtu mtega ndesi. Mtu mtega ndesi kulla siku kazi yake ni hii bassi, akaja mtu Tulatugawe akamwambia: mataka tugawe sawa kwa sawa. na mtu huyo zamani kazi yake kunyanganya watu wa burre bassi, mtu mtega ndesi akatetemeka sana, bibi zake wawili binti Mizabi na binti Saldi, binti Saidi akanena: »tufuate bwana wetu.« na binti Mizabi akanena: »sababu nini? nyama ya ndesi unakula pekeyako. sasa mwanamme wako akakamatwa na Tulatugawe unasema: »twende, tufuate mwanamme wetu. mbona nyama ya ndesi husemi: njoo tugawe sasa. « bassi, binti Saidi akanena: »haizuru lakini mwake atakae mponya

»7 kìlla siku nyama ya ndesi zako.« binti Mizabi asinene neno. kwenda hatta mwituni binti Saidi akarudi mbio, sababu ya kuogopa Tulatugawe. binti Mizabi akamwonaTulatugawe, akamtaka bwana wake na Tulatugawe akampa. mtu mtega ndesi akanena: »sasa mimi nikatwaa bibi wawili, nikipata nyama ao vitu vingine nitawagawia sawasawa. sababu mwanamke yatakayo kuponya hamjuwi. MUamx 0mari bin Ali Kidai

bei

Tunttnijuu.

30. Maskini na mtoto wake. Mtoto akamuliza mama yake: »mama, baba alipokufa, kazi yake nini? sababu mimi mtoto mwanamme dasturi kufanya kazi.« mama yake akanena: »kazi ya baba yako kutega mit ego.« mtoto wa waskini akaenda kutega mitego, akakamata ndege nzuri sana, mtoto wa maskini akamweka barazani kwake. marra akapita mtoto wa sultani akanena: »ndege huyo nzuri sana.« ndege akanena: »mimi si nzuri; nzuri kibibi binti Hutampata na Mayakayaka.« mtoto wa sultani akanena: nini?« ndege akanena: omwambieni mtoto wa maskini«. mtoto wa sultani akamwambia mtoto wa maskini, akaenda hatta njiani akakuta watoto wa sultani wanagombea marisi vitu vitatu kitanga na bilika na sakani. kitanga kana unataka kusafiri utaingia ndani kitakupeleka mbali sana, na bilika inatoka maji na sahani inatoka chakula bass. na binti Mayakayaka ana mtumwa wake jiña lake tumbo, yule mtoto wa maskini akanena: mipeni mimi kitanga na bilika na sahani.« watoto wa sultani wakampa vitu vyote. mtoto wa maskini akaenda hatta kwa binti Mayakayaka. mtoto wa maskini akanena: mimefuata wee.« binti Mayakayaka akanena: »ukimshibisha tumbo bass. na mimi binti Mayakayaka utanipata.« mtoto wa maskini akampa vyakula; tumbo akashiba sana na binti Mayakayaka mtoto wa maskini akampata sababu ya kutega mitego. mtoto wa maskini akapata laha kubwa sana, amefuata kazi ya baba yake. Mkami Katongo bin Salim JTitimbwiii

bei

Tttntinguo.

31. Simba na nyoka. Simba na nyoka wakapigana sana, nyoka akashindwa, akakimbia kwa bin Adam, akamwambia: bin Adam niponye, nataka kuliwa na simba, bin Adam akamwambia: verna; Archiv f. d. Stud. deutsch. Kolonialspr.

Bd. XII.

2

i8

akamficha katika mtungi wa maji. simba akaenda kwa bin Adam, akamwuliza: umeona nyoka hapa? bin Adam akasema: sikumwona. simba akasema: rukhsa kutafuta katika nyumba yako? bin Adam akasema: rukhsa, tafuta katika nyumba yangu; ukimwona utamchukua bassi. simba akashindwa, akenda zake. nyoka akasema: akhsante sana, bin Adam, kwa ajili ya kuniponya; lakini tafazali ñipe rukhsa niende kwangu. bin Adam akamfungulia nyoka, nyoka akauliza: mtenda mema hulipwa nini? bin Adam asema: mtenda mema hulipwa feza; lakini wewe nyoka huna feza; ukiuwa nyama polini ñipe, mimi niliyekuponya katika hatali yako. nyoka akasema: vyema; lakini kujua kwangu mimi nyoka mtenda mema hulipwa maovu; sosa wewe, bin Adam, nitakumeza. kama hupendi kumezwa, túkaulize kwa nyuki. Wakauliza nyuki, akasema: kweli, mtenda mema hulipwa maovu, maana mimi nyuki, nimeweka asali, wana Adam wakanichoma na moto, kwa ajili ya wema wangu. Tena bin Adam akasema: twende pengine. wakenda kwa mwem.be; mwembe akasema: kweli, mimi nawapa matunda killa mwaka; lakini wananikata na kunitupa motoni. bin Adam hakusadiki. wakaenda kwa mnazi wakauliza mnazi, akajibu: kweli, mtenda mema hulipwa maovu, sababu bin Adam wanapata kwangu mnazi nazi na madafu, tena wanikata kwa makuti ya nyumba. bassi, nyoka akasema: sasa ntakumeza. bin Adam akasema: vema; lakini twende nikampe mke wangu buriyani, halafu nimeze. akafika kwa mke wake, akampa buriyani: mke wangu, sasa nitamezwa na nyoka. mkewe akatwaa mayayi, akatia ndani ya kikapo, ale, halafu amle mumewe. nyoka akatia kichwa katika kapo, ale mayayi, mwanamke akamkata kwa upanga, akafa. mume akakasirika sana, akampa taraka kwa sababu: mtenda mema hulipwa mabaya. Soy Riéati atts BHlígch- Uyanda. 32.

Shairi.

Nitakwenda Maskati kwa mji wa katikati, hanunue tende kwa nyama ya mshikaki. utakufa kwa mfundo utakalo hulipati.

19

33. Shairi. Nilipokuwa siwezi hukuja kunitazama, walizani nitakufa, úpate kunila nyama. leo nimeondokea unakuja himahima, wewe si mtu mzuri wala huna horuma. usiingie nyumbani, kaa hapo hapo.

34. Hadisi ya sultani

Mnyanya.

Alikuwa sultani Mnyanya; katika inchi y'ake kulla siku siku y a hokumu. katika nyumba yake juu na chini huweka vyoo. akaweta watu katika nyumba ya hokumu. kulla mtu akatazama juu na chini, akawauliza watu wote: mnaona nini? wakasema wale watu: tunataajabu sababu tunaona watu juu na chini, akawaambia: sasa mmetazama nyumbani kwangu, kulla mtu atatoa elfu dinar, watu wakatoa elfu dinar. Hatta siku moja akaja mtu moja jina lake Mnyanya katika baraza. sultani akamwambia: karibu. akaingia ndani akamtolea salaam, sultani na mawaziri na watu wake wote wakaitikia salaam, akakaa katika baraza wakamwambia: jina lako nani? akawaambia: jina langu Mnyanya. sultani akamwambia: unaona nini? akasema: ninaona uso wangu. akamwambia: unaona wake wangu? akasema: mimi nnaona uso wangu na watu wako. akamwambia: utatoa elfu dinar, akasema: mimi sitoi, sababu nnaona uso wangu. Sultani akamwambia: sababu watu wangu wameona wake wangu, kulla mtu nikamtoza elfu dinar, na wee utatoa vilevile. akamwambia: mimi ninaona uso wangu, simwoni mkeo. sultani akamwambia: nitakupa vitu vitatu upeleke kwa mtoto wangu, vikafika salaama hivo vitu, nitakupa elfu dinar, kama havikufika utakufa. Mnyanya akasema: marahaba bwana wangu. Akampa vitu vitatu: chui na mbuzi na majani, chui asile mbuzi wala mbuzi asile majani. akasema Mnyanya: marahaba bana wangu. Akampa vitu vitatu, akenda yule Mnyanya hatta akafika katika mto na mto mkubwa. akafikiri: nitafanya hila gani 2*

20 mimi Mnyanya hatta niweze kuvusha vitu kivi? akavusha vitu viwili, àkaona nimekufa. akakaa, akafikili katika mtumbwi; akapakia mbuzi na majani katika mtumbwi hatta ngambo akaweka majani, akapakia mbuzi akenda naye ngambo akamfunga, akapakia chui, akenda naye ngambo, akawaza rohoni mwake, akachukua safari yake. Akenda kwa mtoto wa sultani, akapeleka vile vitu vitatu, vikafika salaama. akapewa majibu kupeleka kwa sultani: vitu vimefka salaama, vitu vyote vitatu; majani hayakuliwa na mbuzi, na chui hakula mbuzi, akapewa elfu dinar, sultani akamweka katika inchi yake. Akiia Saìim von uagogoni.

35. Hadisi ya fàkiri mmoja. Alikuwa na mkewe akazaa naye mtoto mmoja mwanamme akapewa mabata yake saba yule mtoto marna yake akaweka fakiri. akatafuta mwanamke maona yeye akaona mwanamke, akatwaa iena, akazaa naye mtoto. yule mwanamke akaweka hawara wake, na mtoto akamwona yule mwanamme, akamwambia: marna hicho chakula unapeleka wapi? baba yangu anafanya kazi huku, wée unapeleka huko kulla siku. yule mtoto wa fakiri kulla siku anaona marna yake anapeleka chakula kwingine. yule mwanamke akaona uzia, yule mwanamke akenda katika mzim kumwapiza afe ao apofoke macho yake. Mtoto akasikia, akatangulia katika mzim. mwanamke akenda mzimni, akasema: nimekuja kwako wewe mzim mtoto wa mume wangu ananiuzi sana; nataka afe ao apofoke macho yake. yule mtoto yuko nyuma ya mzim kazi yake kutikia amina, yule mwanamke akafurahi sana. Hatta alipofika nyumbani mtoto akatia ugonjwa akamwambia: marna yangu, mimi siwezi macho sana, yanatoka machozi marna wake alimwambia: utapona. akatoka yule mwanamke akenda nje kumwambiajyule hawara yake: yule mtoto sasa kaoni, akamwambia: twende nyumbani. yule mwanamke akafuatanalnaye yule mwanamme akaingia naye ndani akamweka katika mbuzi. yule mtoto akamwambia: huyu mtu gani aliokaa hapo? yule mwanamke akamwambia: yuko wapi mtu? yule mtoto akasema: huyu hapo. yule mwanamke akamwondoa, akamtia katika kikanda. yule mtoto akachukua kile kikanda kwa sultani, sultani akamwambia: nini hicho? yule mtoto akasema: nataka kasiki ilio ndani, na mimi nikupe kikanda.

21

sultani akamwambia: toeni hiyo kasiki ilio ndatii, lena wakatoa. walipotoa kasiki ndani mna mwanamme. na lile kanda likajunguliwa ndani mna mwanamme. Sultani akauliza: nani huyu? yule mtoto akamwambia: huyu ndio anakwisha vyakula vya baba yangu vyote. Tena sultani akasema: hawa wezi na mimi nimewaona nyumbani kwangu. sultani akaamru kwenda kutoswa baharini. Akida Salim fon

ìiagogùni.

36. Hadisi. Kapo la matundu manne nikachumie mbaazi, Mwarabu akenda shitaki tuhukumiwe kwa hakki. kapewa wingi wa mali na pembe mbili za nyali; mtasema mtachoka: binti Saidi simwachi. S. b. J.

37. Shairi. Marisuku, marisuku, upere si ukurutu, pwani maji kukutu, nitukane kwa mato, kwa jina hunisubutu.

s. ì>. J.

38. Shairi. Wingu la mvua likanya nili kwa mama mkuu hapanda miti miwili, muhinna na mtambuu, mtambuu hatafuna, muhinna hoska miguti. usinione mdogo, moyo wangu wa kikuu. S. b. J.

39. Maskini. Maskini hana jembe wala hana mdu. maskini akanena: ntalima kwa mikono. alipokwisha lima, akapanda kunde, zikaota. zilipozaa nyingi, akachuma akakaa pattali kuna gogò, kuchambua kunde kutaka kula kunde zikamwagika zikaingia ndani ya gogò.

22

Maskini yakenda kwa skoka, na shoka yakenda kwa moto, na moto yakenda kwa maji; na maji mzima moto, na moto tnchoma shoka, na shoka mpasua gogo, na gogo likatoka feza nyingi sana, tena maskini akawa Saldi kukaa kishiwa cha Unguja na yule shoka kukaa mlima sababu ndio aliompa usuitani, hana budi kuwa hakida wake na hokumu ndogo kwake shoka. lakini Saldi zamani maskini sasa tajiri. Maanayake ndio watu wabarra wakipendakulima wakakosa kusoma na kazi nyingine, sababu sultani wao amepata mali kwa kulima; lakini watoto wa sasa hawana akili ndio maana wasipate mali wakawa maskini sababu wameacha amri ya sultani ya kulima na mikono na kupanda kunde. zamani dasiuri ya kikami kupanda kunde. bassi. marni ir«™ Kiaanga. 40. Ali na mtoto wake Salini. Salim akanena: mimi nataka bibi mpokea mikwaju. mwanamke moja akanena: huyo Salim nasikia anataka bibi mpokea mikwaju, kweli? watu wakanena: kweli. bibi akanena: yaje aoe mimi. Salim akasikia huko kwa sultani yuko bibi mpokea mikwaju. Salim yakenda hatta kwa bibi akamwoa. Salim akanena: bibi iname, upokee mikwaju. bibi akanena: Salim, dasturi gani, umetoka juani wala hatujafanza chakula wala wataka nipokee mikwaju? Salim akasema: kweli. Hatta kwa siku ya pili Salim akatoka kutembea, akanena: bibi iname upokee mikwaju. bibi akanena: wewe Salim una wazim? ukasikia mtu apiga bibi yake yule mwanamme na wajakazi na watwana. Salim akanena: kweli, na mimi Salim sina budi kwenda barra. Ndiyo maana Waarabu wakasafiri sababu ya wanawake. Salim alipokwenda barra, akafa, sababu Salim alisema: nikipata wajakazi na watwana ntapata kumpiga bibi yangu. Mknmai Mztru. 41. Mtu mjuga

mbuzi.

Mtu mjuga mbuzi alikuwa na mbuzi wengi sana; lakini mbuzi moja alikuwa hawezi vidonda siku nyingi sana, bwana wake akanena: Kitola nenda kamtupe mwituni. Kitola yasiende kumtupa. bwana wake akenda kumtupa. mbuzi akakaa siku nyingi mwituni, vidonda vikapona. mbuzi kule mwituni

23

akazaa watoto wengi sana, bwana wao akapata habari kama: mbuzi wako ana watoto wengi sana, bwana wao akauliza: mbuzi gani? Salim akanena: yule uliyomtupa. bwana wao akanena: nitamfuata. kwenda hatta polini akakuta mbuzi wengi sana, mala mbuzi moja akamwona yule mtu mbuzi aliyo mkubwa akanena: yule bivana sasa na twende tukamwue. mala bwana akafa. marni Sa Idi Un Saii. Kisanga.

42. Funài. Fundi mpiga nyama alikwenda polini alikuta ngombe anakula majani makavu. fundi kurudi nyumbani akanena: baba, mimi fundi nimeona ngombe hula majani makavu; maana yake nini? baba akanena: tajiri hula faida, fundi akasema: kweli. maskini Tena akenda polini marra ingine, akamkuta aliofunga kuni nyingi sana, kutaka kuweka kichwani haziwezi; tena kutwaa ingine kuongeza. fundi kurudi kwa baba yake akanena: baba mimi fundi nalimkuta polini mtu aliofunga kuni. kutaka kuweka kichwani haziwezi; maana yake nini? baba yake akanena: mtu mwenyi malata malata yale hayajesha marra hutaka mengine. fundi akasema: kweli. baba yake akanena: ukasikia tajiri hula faida sababu majani mabichi ndio mali na majani makavu ndio faida; ukisema nile majani mabichi ndiyo faida majani makavu. mami Tebe. Kisanga.

43. Sungula na watu. Watu ivaliopika vyakula vingi sana kashata na mandasi na tambi na bajia na mkate na asali na haruwa na wali na sukari na nyama ya ngombe na nyama ya kuku na bota na samaki na njiwa, killa kitu chà duniani watu wakanena: sungura nenda kajaribu vyakula na nyama. sungura akanawa mikono miwili kuchota chakula kwa mkono wa kushoto. sultani akanena: kwa nini unachota chakula kwa mkono wa kushoto? sungura akachota kwa mkono wa kulia. alipokwisha jaribu, watu wakanena: chakula kitam nini? sungula akanena: chakula hachiwi kitamu ila ya maneno mazuri. akisema maneno mabaya na chakula kibaya, akisema maneno mazuri na chakula kizuri. Watu wakanena: kweli, mtu akikutukana, huwezi kula chakula. manti Tebe. Kisanga.

24

44. Dalari si verna. Hapo zamani kazi kukata milala polirli, akaona kichwa cha mtu aliyokufa zamani. Dalari kukipiga kichwa kikanena: Dalari si verna, mtu akianguka, mwambie: pole unamwambia: doko ndio ulimwangusha. Dalari akenda nyumbani, akanena: polirti kuria kichwa cha mtu kinasema. watu nyumbani wakanena: wewe mwongo sana. Dalari akanena: mimi tukienda polini kichwa kama hachi kusema niueni bassi, na watu wakakubali sana, wakaenda batta polini, wakakikuta kichwa wakakigonga, kisinene neno. Watu wakanena: sasa Dalari tutakuua, sababu ndio mda wetu. Dalari akafa; kichwa kikanena: umeona, Dalari, mimi kichwa nikanena: mtu akaanguka mwambie: pole. sasa urnekufa kama mimi, watu wakanena: mwenzetu tumemwua burre. sasa ndio maana watu wakianguka husema: pole, sababu mtu alikufa. marni Sue di bin Saidi. Kisanga.

45. Mwongo na makauhiza. Mwongo akasema: nataka kwenda polini. polini akamwona makauhiza aliochukua mtu. mwongo marra akamwona anataka kusema maneno. makauhiza akanena: weye mwongo umeniona; lakini nyumbani usiseme neno. Mwongo alipokwenda nyumbani akanena: bibi yangu, mimi mwongo polini nimeona makauhiza akachukua mtu aliokufa. bibi akanena: sema kweli. mwongo akasema: kweli. bibi akamwambia baba yake, akaja kumwuliza mwongo, akanena: twendeni polini bado mtamwona. wakaenda hatta polini. wasimwone makauhiza wala mtu mwingine. Bibi yake akanena: mkamateni mwongo, tukamwue, sababu mtu mbaya sana huyu ndio aliomchimbua mama yangu kaburini; sasa naye mwueni. Makauhiza kamzulia burre. mami Sue(Ji Wn saia. Kisanga.

46. Simba na mbala. Simba akaenda kwa mganga kiwanya cha kujenga nyumba na mbala akaenda kwa mganga kiwanya cha kujenga; lakini kile kiwanya kimoja. simba anataka kujenga na mbala anataka

25

kujenga. kiwanya kinayotoka kujenga simba na tubala anataka kujenga kilekile bassi. Simba hukata mijengo na mbala hukata mijengo; lakini siku ya kupeleka mijengo simba na mbala kukaa nyumbani, na siku ya kupeleka mijengo mbala na simba kukaa nyumbani. kwa siku ya pili simba akapeleka mijengo akasema: mimi simba hodari sana; mijengo nimeanza jana leo mijengo imejaa tele bassi, kesho nikija nijenge. Kwa siku ya tatú mbala akapeleka mijengo na mbala akanena: mimi hodari sana, kesho nikija ntaleta nyassi. kwa siku ya nne akaenda simba, akakuta nyumba imekwisha jengwa; simba akanena: mimi simba hodari sana, kesho nikija nitahama. Lakini mbala na simba hawajaonana. mbala akahama, simba alivokuja akaona nyumba yake inawaka moto, simba akapiga hodi, mbala akanena: karibu. simba akanena: sababu ya kukaa nyumba yangu. mbala akasema: nyumba yangu. simba akanena: bassi, sasa tukae wote. Ndio maana watu wakakaa nyumba moja watu wawili, sababu simba na mbala waliowaona. Mkami

47. Mtu

na watoto

Selemani bin Tunmiguo.

Mbena

wake.

Mwaka wa njaa baba yao akawapa vijiko, watoto wakanena: sisi watatu vijiko vya kulia mboga. na watoto wawili wakanena: vijiko vyetu vya kulia nyama. baba yao akanena: ondokeni sababu mwaka huu njaa nyingi sana, mnataka nyama na ugali. watoto wakaenda zao polini wakakuta vyakula vingi sana na nyama wengi sana, watoto wawili wakapata mali nyingi sana. Baba yao akasikia: watoto wako wana mali nyingi sana, na baba yao akawajuata watoto wake. watoto wakanena: baba weye, ndio uliosema: nyinyi nendeni polini sababu mkataja vijiko vya kulia ugali utakuwaje kutufuata? baba yao asinene neno akanyamaza kimya. watoto wakanena: baba mjinga sana; killa mtoto wako mwenyewe ukamfukuza, sasa haizuru ukae bassi. Maana yake mtoto wako japokuwa mjinga sana haifai kumfukuza sababu utakosa amri ya watoto wako. Mkami

Mrisho bin Kisanga.

Ali

26 48. Salim na bibi yake. Salim akanena: mwaka wa kufa weye bibi yangu tutazikwa pamoja na mimi Salim. kwa mwaka mwingine bibi yake akafa. Salim akanena: sasa tutazikwa. wote watu katika inchi wakanena: kweli, wamependana sana, kwenda kaburini shetani amemwuliza kuliliwa? Salim akanena: sikuliliwa. shetani akanena: mtu dunyani kama hakuliliwa hapati kuzikwa pamoja. Salim akarudi nyumbani; watu wakamwuliza. Salim akanena: mtu kama hakuliliwa hapati kuzikwa pamoja na mtu alioliliwa. kama wakaliliwa wote walina bibi yao lakini mtazikwa mbalimbali, killa mtu ana kaburi yake.. lakini zamani kama mtu na bibi yake wakapendana huzikwa pamoja, lakini sasa killa mtu ana kaburi yake. lakini watoto wa sasa wakanena: mbona wanawake hawana uhadi ndio maana wakakosana na wanawake, wanawake watu wabaya sana. Mkami

Tebe bin Kisanga.

Salim

49. Kahaba na chawivu. Kahaba kazi yake kutongoza bibi za watu; lakini chawivu bibi yake hapati rukhsa kwenda tembea, sababu akitembea atamtongoza kahaba. hatta siku moja chawivu akanena: bibi yangu nenda katafute kuni. marra kahaba yakamwona bibi wa chawivu, kahaba akamtongoza. bibi akanena: mimi sitaki, sababu mwanamme wangu chawivu. kahaba akanena: mimi nitamtoa wivu. bibi akanena: mimi ukamtoa wivu utanioa weye kahaba. kahaba akanena: wee bibi, leo unapika mboga gani? bibi akanena: nimepika samaki. kahaba akasema: bassi. Hatta usiku kahaba akachukua samaki wazima. bibi alipopeleka ugali na kitoweo, kahaba akatumbukiza samaki wabichi. chawivu akichota tonge la chakula kuchukua samaki, samaki wafanza nguvu. chawivu akanena: bibi weye sasa sikutaki sababu mtu mbaya sana, kahaba akapata bibi sababu ya akili za ukahaba. Mtu mkahaba si mzuri kazi kuvunja nyumba za watu. mtu mkahdba haifai kukaa inchi ya barra, afaa kukaa Dar-es-Salam ao Bagamoyo sababu bibi tele bass. ukahaba hupatani na mtu bassi.

Mkami

Tebe bin Kisanga.

Salim

27

50. Mtu mtega

mitego.

Killa siku hunasa nyama nyingi sana; lakini dudu inakula nyama. mtu mtega mitego akanena: ntamvizia. yakamwona dudu akamfukuza hatta kwa jundi wa matendegu. dudu likanena: niponye. jundi akanena: ingia tumboni. dudu likaingia. mtu mtega mitego alipofika kwa fundi, akanena: dudu umeliona? fundi akanena: sikuliona. mtu mtega mitego akaenda zake. dudu likatoka, likanena: fundi mimi nataka nikutafune. jundi akanena: mimi wema wote nimejanza; lakini ningoje nikaulize. Akaenda hatta kwa watu wakubwa, jundi akanena: minti nimemponya dudu; lakini sasa dudu lataka kunila maana yake nini? watu wakanena: mwema moja. fundi akanena: kweli bassi; sasa nitakwenda kwa bibi yangu. alipofika kwa bibi yake, fundi akanena: dudu lataka kunila. bibi akanena: shika mkate, mpelekee dudu. fundi akampa dudu, dudu likala mkate, likafa. fundi akanena: bibi yangu mbaya sana, sasa sikutaki. bibi yake akanena: mbona, dudu lalitaka kukula; sasa mimi ni mbaya. Watu wasema: kweli, mwema moja. Mkami

51. Bunuwasi

na

Tebe bin Kisanga.

Salim

mfaume.

Bunuwasi akanena: mfaume bibi yako mkubwa anazini na kitwana chako. mfaume akanena: sema kweli. Bunuwasi akasema: kweli. mfaume alipokwenda nyumbani, yakamkuta bibi yake mkubwa anazini na mtwana. mfaume akanena: Bunuwasi si mtu mzuri, afazali mkamtupe baharini, sababu na mimi nikazini na bibi yangu, Bunuwasi ataniona. mfaume akamtwaa Bunuwasi, akamtia ndani ya kanda, akaenda hatta baharini; akakuta pwani maji yamekwenda mbali. mfaume akanena: mwacheni hapo, maji yakirudi, tutamtupa. Aliporudi nyumbani mfaume, marra akapita sultani, akanena: weye ndani ya kanda nani? Bunuwasi akanena: mimi nakwenda oa binti Saldi, sultani akanena: toka niingie mimi sultani. Bunuwasi akanena: mfaume mtu mbaya sana, mimi Bunuwasi nalimwambia vyema lakini kwake vibaya. Hatta siku ingine Bunuwasi akaenda kwa mfaume. mfaume akanena: weye Bunuwasi mtu mzuri sana, sababu, ukiona neno,

28 husema. ndio maana watu wàkawa na wivu sababu ya Bunuwasi. zamani mtu akizini na bibi ya watu Bunuwasi hujua. Mkami Koka bin Kìèanga.

Mayata

52. Mtoto wa maskini.

Mtoto wa maskini alitaka kazi. boba yake akampa kazi ya kulima. mtoto akaona, kazi ya kulima haìna faida, boba yake akampa kazi ya kuvua samaki. na mtoto akaona kazi ya satnaki haìna faida, boba yake akampeleka kwa funài wa kwiba. mtoto wakamfundisha kwiba. Mtoto alipohitim kazi ya kwiba, siku moja akapita mtu aliyechukua mbuzi. mtoto wa maskini akanena: mafundi twendeni tukebe. mafundi wakanena: sisi twajua kwiba usiku. mtoto akanena: mimi nakwenda kwiba. mtoto akapata mbuzi. aliporudi nyumbani kwa mafundi, mtoto akanena: kuleni nyama, utumbo niwekeni vyema. lakini mafundi walikula nyama na utumbo. Mtoto akanena: mimi sasa, marna, nitawebia mafundi. marna yake na baba yake wakanena: sisi kazi yenu hatujui. mtoto wa maskini kutimia saa sitta za usiku, mtoto yakawebia mafundi. hatta asubuhi mafundi wakaona vitu vimeibiwa. mafundi wakanena: na twende kwa sultani tukebe. mtoto yakaenda hatta kwa sultani, mafundi walipofka kwa sultani, mtoto yakawapiga bunduki. mafundi wakafa wòte, sababu kazi ya kwiba mbaya sana. „, ìlkami Tebe b. Sahm. J

J

53. Mtoto maskini. Mtoto maskini hana baba; mtoto akanena: mimi sasa maskini, nifanye kazi gani? labda nikatege mitego. kama nikapata ndege nipate kula, sababu sina baba. mtoto akaenda hatta mwituni akatega mtego wake moja akaenda nyumbani. asubuhi akaenda tazama mtego akamkuta mzee: mtoto maskini akanyamaza, asinene neno. mzee akanena: mtoto njoo utwae kikombe; lakini kikombe usimpe mtu, sababu mna mali nyingi na killa kitu. mtoto akafurahi sana, yakapata utajiri bassi. Mkami Kopa Mn Kùanga.

iflango

54. Mtu mchimba kàburi.

Zamani inchi yote mchimba kaburi mtu moja. kwa kuchimba kwake zayidi akapata jiwe. yeye mchimba kaburi jiwe akampa

29 sultani, alipokwisha mpa jiwe likatoka feza. na sultani akampa kibibi binti sultani akamwambia: mchimba kaburi tutu mzuri sana, afaa kutnpa kibibi binti sultani. Na yeye mchimba kaburi yakapata usultani kwa sababu ya kuchimba kaburi. ,„ . „ .. ,„ MKtimi Kopa om Miangtt Kisa nga. 55. Mbetembe na bubu. Mwaka moja mbetembe na bubu wakenda polini wakaokota nyama na nyoka. mbetembe hula nyama nzuri, bubu humpa nyoka, sababu hana macho, bubu marra akapata macho tena bubu akasema: wee mbetembe mbaya sana; lakini haizuru twende polini tukachimbe panya. kwenda polini bubu akanena: mbetembe ningoje hapa mimi kwenda kutwaa moto, bubu akachoma moto majani. mbetembe kuona moto unawaka, yakapiga kelele nyingi sana, marra akapata miguu. Mbetembe akampa macho bubu, na bubu akampa mbetembe miguu. marni Kopa tin Mhnuj,, Kisongo. 56. Maskini

na mtoto waìce.

Maskini akanena: mwaka nitakaokufa chukua mbegu za maboga kapande kaburini kwangu na wewe mwanangu utakuwa tajiri sana, mtoto yakakubali sana, alipokufa akachukua mbegu kwenda panda, lilipozaa, mtoto maskini kupasua boga ndani likatoka feza nyingi sana, mtoto maskini akapata utajiri kwa sababu amefuata amri ya baba yake. ,„ . „ Kopa ,. ,„ ' Mkami bin Mìango. 57.

Kibwana.

Kibwana mtu wa ila sana, baba yake akanena: Kibwana nikuoze mke. Kibwana akanena: ningoje niende pwani. baba yake akanena: haya nenda. Kibwana akaenenda hatta mjini akafika kijana mwanamke mzuri sana, kibwana akanena: kijana mimi nakutaka nizini nawe. kijana mwanamke akanena: ningoje niende sokoni nikanunue mchele nikampikie mwanamme wangu, bassi; saa sitta ntakuja utazini nami. Kibwana akaona ujanja wa wanawake, akarudi nyumbani kwa baba yake, akanena: baba mimi Kibwana nataka bibi. baba yake akamwoza bibi.

30 Siku moja katika saa sitta bibi akanena: Kibwana mimi mama yangu akaniagiza leo saa sitta za mchana nende kwao. Kibwana akanena: sitaki sababu mimi Kibwana nilipokwenda pwani kijana mwanamke nimetongoza, akanena: ngoje saa sitta. sasa weye bibi yangu wataka kwenda kwa mama, huna rukksa.

Mkami Kibwana bin Selemani Kikundi kwa Sadi.

58. Sika na Salim na Bende. Sika naSalimna Bende watu hao wote baba yao moja, watoto wakanena: baba sisi twataka kusafiri kutafuta dawa. baba yao akanena: verna, tena killa mtoto amepata feza; lakini Bende akapata mishale kumi. wakapata safari hatta njiani. Bende akaona mtu alio majani kugeuka nguo. Bende akanena: mimi nataka kuuliza dawa hii. mpika nguo akanena: nipe mishale miwili. Bende akampa, mpika nguo akampa dawa. Bende akaenda hatta mbele akaona mtu aliopiga mkuki bibi yake. Bende akanena: dawa gani hii? mtu aliopiga mkuki bibi yake akanena: dawa ya kumpiga bibi yako utapata kulima shamba kubwa sana. Bende akanena: na mimi nataka dawa hii. mtu mpiga mkuki bibi yake akanena: weye unataka dawa? Bende akanena: nataka. mtu mpiga mkuki akanena: nipe mishale minane. Bende akapata dawa. Kurudi nyumbani akapika majani, akapata kugeuka nguo nyingi sana, tena akapiga mkuki bibi yake Bende na Bende akapata mali nyingi sana. Sika na Salim, waliopata mali nyingi sana kwa baba yao, lakini njiani hawakupata dawa; tena wakakosa mali. Bende akapata mali, bassi. mami Tebe Mn SaMi Kiaanga.

59. Pendo na mwanamme. Pendo akanena: weye mwanamme mwaka wa kufa tuzikwe pamoja. mwanamme akanena: hatta mimi, mwaka wa kufa, pendo, tutazikwa pamoja. hatta mwaka mwingine pendo akafa, mwanamme akanena: pendo leo alipokufa shurti tuzikwe pamoja. watu wakanena: hatujaona mtu aliokufa akazikwa na mtu alio mzima. mwanamme wa pendo akanena: sababu mimi na mwanamke naliweka wahadi sasa pendo amekufa, sina buddi kuzikwa na bibi yangu. watu wakanena: kweli, sababu uhadi mbaya sana, na twende tukawazike pamoja.

31

Walipokwisha zika mda wa siku sitta akaja shetani, akampa dawa, pendo akafnfuka pamoja mwanamme. kurudi nyumbani mwanamme akanena: bibi ningoje hapa mimi nikatwae nguo. pendo akasema: verna, mwanamme kwenda nyumbani marra akapita Mwarabu, akamtwaa bibi yake. mwanamme kurudi yakamkuta hapana. mwanamme akanena: pendo hana uhadi. Maana yake mwanamke kana akisema, mimi kufa na wewe uzikwe pamoja, usisadike kabisa, sababu wanawake marra ... .